- BREAKING NEWS: TANZANIA YAKANUSHA KUWASHIKILIA KINA DR SLAA NA MWAMBUKUZI
- BREAKING NEWS: RAIS WA MAPINDUZI WA NIGER AMTEUA WAZIRI MKUU MPYA
- BREAKING NEWS: SHILINGI YA KENYA YAPOROMOKA VIBAYA DHIDI YA DOLA
- BREAKING SEREKALI YA RWANDA YAKASIRISHWA NA UBELGIJI KUTOMUIDHINISHA BALOZI WAKE
- BREAKING NEWS: RAIS KIM AKUTANA NA WAZIRI WA ULINZI WA URUSI
BURUDANI: USHAURI WA DIAMOND KWA WASANII WENZAKE
Mwanamuzi staa wa Bongo flevani nchini Tanzania Naseeb Abdul, maarufu kama ‘Diamond Platnumz’ amewataka wasanii wenzake kutumia vivutio vya Taifa katika kazi zao ili kutangaza utalii uliopo nchini.
Diamond Platnumz amejisema kwa upande wake binafsi yupo tayari kutangaza vivutio mbalimbali kwa ajili ya kuitangaza nchi yake kupitia kazi zake.
“Haiwezekani mastaa kutoka nchi zingine kutembelea vivutio vyetu wakati sisi wenyewe tupo karibu na tunashindwa kwenda, mastaa wengi wamekuja nchini kama vile David, Beckham, Lionel Messi wamepanda mlima wetu Kilimanjaro.
“Nimefurahi kupanda Kilimanjaro japokuwa sikufanikiwa kufika kileleni, lakini kwangu ni jambo la kubwa na historia, hivyo wasanii kupitia kazi zetu inabidi tutangaze vivutio vyetu ili watalii waje, nchi ijulikane na tukuze uchumi wetu,” alisema msanii huyo.