Home | Terms & Conditions | Help

May 3, 2024, 7:56 am

NEWS: RAIS KIM AKUTANA NA WAZIRI WA ULINZI WA URUSI

Rais wa Korea Kaskazini Kim Jong Un leo amekutana na waziri wa Ulinzi wa Urusi Sergei Shoigu kujadili masuala mbalimbali ya kijeshi na mazingira ya usalama wa kikanda.

Mjumbe huyo wa Rais Vladimir Putin amekutana na kiongozi wa Korea Kaskazini wakati ambapo nchi hiyo iliyojitenga na mataifa mengine ulimwenguni ikiadhimisha miaka 70 tangu vita vya Korea vya kati ya mwaka 1950-1953 vilipositishwa.

North Korea's Kim meets with Russian defence chief Shoigu in Pyongyang

Katika mkutano huo, Shoigu anaripotiwa kumuwasilishia Kim barua "nzuri" iliyotiwa saini na Rais Vladimir Putin.

Hata hivyo, haikuwekwa wazi masuala ya kijeshi yaliyojadiliwa katika mkutano wa viongozi hao wawili.

North Korean leader Kim Jong Un meets Russian defence minister Sergei Shoigu, both sides pledge to boost ties | Mint

Korea Kaskazini imekuwa ikiiunga mkono Urusi katika vita vyake na Ukraine ikisema nchi za Magharibi zinazoongozwa na Marekani, ndizo zilizoipelekea Urusi kuchukua hatua za kulinda maslahi yake ya kiusalama.

Kim Jong Un amemuonyesha silaha za kisasa zaidi za Korea Kaskazini mkuu wa ulinzi wa Urusi Sergei Shoigu.

Utawala wa Pyongyang uliualika ujumbe wa Urusi unaoongozwa na Bw Shoigu, pamoja na maafisa wa China.

Watahudhuria sherehe za Pyongyang za kumbukumbu ya miaka 70 ya uwekaji silaha wa Vita vya Korea, inayoadhimishwa kwa gwaride kubwa la kijeshi.

Silaha zilizoonyeshwa ni pamoja na kombora la balestiki la Hwasong intercontinental (ICBM).

Silaha hii ilijaribiwa kwa ufanisi mwezi wa Aprili, na inaaminika kuwa ina uwezo wa kurushwa kwa haraka kulenga eneo lililokusudiwa.

Pia kwenye onyesho hilo kulikuwa na miundo miwili mipya ya ndege zisizo na rubani, ikiwa ni pamoja na moja inayofanana na ndege isiyo na rubani ya msingi inayotumiwa na Jeshi la Wanahewa la Marekani, kulingana na NK News, tovuti maalum inayoangazia Korea Kaskazini.

Ziara hiyo ya kirafiki inajiri huku kukiwa na shutuma kwamba Pyongyang inaipatia Urusi silaha kwa ajili ya matumizi katika vita vyake nchini Ukraine - madai ambayo Pyongyang na Moscow zinakanusha.

Korea Kaskazini ilisema Bw Kim na Bw Shoigu walijadili "mambo ya kuheshimiana" katika nyanja za ulinzi wa taifa na mazingira ya usalama wa kimataifa.

Ziara ya wajumbe hao kwa ajili ya Siku ya Ushindi ya Korea Kaskazini - kama vile mwisho wa uhasama wa 1953 inavyoitwa Kaskazini - inatarajiwa kukamilika siku ya Alhamisi kwa gwaride kubwa la kijeshi. Kitaalam Korea bado wako vitani kwa sababu hakuna makubaliano ya amani yaliyofikiwa mzozo ulipoisha.